Customise Consent Preferences

We use cookies to help you navigate efficiently and perform certain functions. You will find detailed information about all cookies under each consent category below.

The cookies that are categorised as "Necessary" are stored on your browser as they are essential for enabling the basic functionalities of the site. ... 

Always Active

Necessary cookies are required to enable the basic features of this site, such as providing secure log-in or adjusting your consent preferences. These cookies do not store any personally identifiable data.

No cookies to display.

Functional cookies help perform certain functionalities like sharing the content of the website on social media platforms, collecting feedback, and other third-party features.

No cookies to display.

Analytical cookies are used to understand how visitors interact with the website. These cookies help provide information on metrics such as the number of visitors, bounce rate, traffic source, etc.

No cookies to display.

Performance cookies are used to understand and analyse the key performance indexes of the website which helps in delivering a better user experience for the visitors.

No cookies to display.

Advertisement cookies are used to provide visitors with customised advertisements based on the pages you visited previously and to analyse the effectiveness of the ad campaigns.

No cookies to display.

UGONJWA WA MPOX ULIVYOGUNDULIKA TANZANIA

0
image
Ads

Tanzania imethibitisha kesi mbili za ugonjwa wa Mpox baada ya uchunguzi wa maabara kuthibitisha uwepo wa virusi hivyo kwa wahisiwa wawili. Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, ametangaza taarifa hiyo leo, Machi 10, 2025, akieleza hali ya ugonjwa huo nchini.

Kwa mujibu wa Waziri Mhagama, Wizara ya Afya ilipokea taarifa za wahisiwa mnamo Machi 7, 2025, kupitia mifumo yake ya ufuatiliaji wa magonjwa. Wahisiwa hao walikuwa na dalili kama vipele vilivyojitokeza usoni, mikononi, miguuni, na sehemu nyingine za mwili. Aidha, mmoja wa wahisiwa ni dereva wa gari la mizigo aliyesafiri kutoka nchi jirani hadi Dar es Salaam.

Baada ya kuchukua sampuli na kuzipeleka Maabara ya Taifa kwa uchunguzi, majibu yaliyotolewa Machi 9, 2025, yalithibitisha kuwa wahisiwa hao wawili wameambukizwa virusi vya Mpox.

Ads

Hatua Zinazochukuliwa na Serikali

Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI na vituo vya kutolea huduma za afya, inaendelea na ufuatiliaji wa ugonjwa huu ili kubaini wahisiwa wengine na kuwapatia huduma stahiki. Serikali pia inaimarisha juhudi za kudhibiti maambukizi kwa:

✅ Ufuatiliaji wa magonjwa katika ngazi zote
✅ Upimaji wa wasafiri wanaoingia na kutoka nchini
✅ Kuongeza elimu ya afya kwa umma kuhusu kujikinga na maambukizi

Chanzo cha Maambukizi na Njia za Kujikinga

Mpox husababishwa na virusi vinavyopatikana kwa wanyama wa jamii ya nyani, na binadamu anaweza kupata maambukizi kwa kugusana na wanyama hao, majimaji yao, au kula nyama iliyoambukizwa. Ugonjwa huu pia huweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia mgusano wa moja kwa moja.

Wananchi wanahimizwa kuchukua tahadhari kwa kuepuka kugusana na wagonjwa, kudumisha usafi wa mikono, na kuripoti dalili zozote zinazohusiana na ugonjwa huu katika vituo vya afya vilivyo karibu.

Kwa taarifa zaidi kuhusu ugonjwa wa Mpox na jinsi ya kujikinga, endelea kufuatilia matangazo rasmi kutoka Wizara ya Afya.

SOMA HII: Virusi Hatari Vinavyotokana na Panya

Spread the love
Ads

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *